Mwongozo Kamili Kwa Wagonjwa Wa Figo
    OKOA FIGO LAKO
    Ujumbe Kamili Juu ya Kukinga na Kuponya Magonjwa ya Figo
    
    
    
    
    
        Dr Gabriel L. Upunda
        Dar es Salaam, Tanzania
    
    Dr Bashir Admani 
Nairobi, Kenya 
         Dr Sanjay Pandya
Rajkot, India
      
                         
                    
                       
                            
                              OKOA FIGO LAKO
    Mchapishaji
TMJ Hospital,Mikocheni, Dar es Salaam, Tanzania
    
    
    
        © Samarpan Kidney Foundation
        Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kukitoa kitabu hiki kwa namna yoyote ile:
        iwe kwa mfumo wa elektroni ikiwa pamoja na mfumo wowote wa kuhifadhi na
        kutoa taarifa, bila idhini ya mchapishaji. Kitabu hiki huchapishwa India na kwa
        hiyo  kisifanyiwe  biasharanje  (exported),  bila  kupata  ruhusa  kwanza  kwa
        maandishi kutoka kwa mchapishaji. Kama kutatokea utata wowote wa kisheria,
        utata huo utasuluhishwa tu chini ya sheria ya Rajkot, India.
    
    
    
    
    Toleo la kwanza  : 2015
    bei:TZS
    
    
    
    
        
            Mwandishi
            Dr Gabriel L Upunda
        
        
            Mganga Mkuu Wa Serikali (Mstaafu)
            Wizara Ya Afya Na Ustawi wa Jamii
            SLP 5720
        
        
Dar es Salaam, Tanzania.
    
    
                         
                    
                       
                            
                            
Kitabu Hiki Kimetolewa Kwa
Ukumbusho Wa Wagonjwa Wote Wa Figo
                        
                    
                       
                            
                            Hebu tujikinge na magonjwa ya figo
Kitabu  hiki “Okoa Figo Lako” ni jitihada ya makusudi ya kutoa
maelezo ya msingi ya jinsi ya kujikinga na magonjwa ya kawaida ya
figo.
Kwa miongo kadha iliopita kumekuwa na mlipuko wa kuogofya na wa
kuongezeka kwa maradhi ya figo.  Magonjwa ya figo yaliyozidi na
yasiyotibika yamekua kwa wingi.  Kwa sababu hiyo kuwaeleza watu
sababu, dalili na mbinu za kujikinga na magonjwa haya ni mbinu bora
ya kupambana na ongezeko hili la kusumbua.  Kitabu hiki ni mchango
wetu wa kujaribu kumpa mtu wa kawaida ujumbe muhimu kwa maneno
rahisi.
Uchunguzi, utambuzi na matibabu ya mapema ya ugonjwa huu ni muhimu
kwa vile humpa mgonjwa manufaa ya gharama ndogo ya matibabu.
Kwa kutokujua watu wachache kabisa hutambua ishara na dalili
zinazoonyesha uwezekano wa kuwa na  ugonjwa wa figo, nao pia
hucheleweshwa kwa uchunguzi na kupewa matibabu kama dialysis au
kubadilisha figo ambayo ni ghali mno na hata katika nchi kama india ni
wachache tu,  kama asilimia kumi (10%) ya wagonjwa wote, huweza
kumudu gharama hizo.  Kwa hiyo uchunguzi na utibabu wa mapema
zinabaki kuwa njia pekee inayoweza  kupunguza mlipuko wa ugonjwa
wa figo uliokomaa katika nchi yetu.
Uchunguzi unaonyesha kuwa mtu akigundulika anaugua ugonjwa wa
figo, mgonjwa na familia yake huwa na mawazo mazito na wasiwasi.
Wagonjwa wa figo na familia zao hupenda kujua kila kitu juu ya ugonjwa.
Lakini  si  rahisi kwa  daktari  anayetibu  kuwapa maelezo mengi.
Tunatumaini kitabu hiki kitajenga daraja kati ya daktari na mgonjwa.
Hata hivyo ni msaada kuwa na kitabu cha maelezo ili husome kwa
wakati wako na kukipitia mara nyingi unavyohitaji.  Kukupa ujumbe
                        
 
                    
                       
                            
                            wote wa msingi juu ya dalili, uchunguzi na matibabu ya magonjwa
mbalimbali ya figo kwa lugha rahisi na nyepesi.  Maelezo ya kuchagua
na jinsi ya kujikinga kwa vyakula vinavyopendekezwa kwa magonjwa
mbalimbali ya figo yote yametolewa hapa.  Tunahitaji kusisitiza na kulenga
kwa kusema hapa kuwa ujumbe unaopatikana katika kitabu hiki si
usaidizi wa kimatibabu; ni kwa kukupa ujumbe pekee.  Matibabu binafsi
au kubadilisha vyakula kwa kusoma kitabu hiki, bila ushauri wa daktari
yaweza kuwa hatari,  hatushauri na haikubaliki kabisa.
Mwongozo huu wa figo utakuwa muhimu si tu kwa wagonjwa wa figo
na famila zao tu bali hata kwa wale waliohatarini  kupata ugonjwa wa
figo.  Na utatoa mafunzo kwa wale watu ambao hupenda kujua..
Madaktari, wanafunzi wa matibabu, matabibu waliofunzwa kusaidia
kutibu, wanahaki ya kupata kitabu hiki ili kiwe msaada wa karibu.
Tunamshukuru sana Mr. Pravin V. Pindoriya na Timu yake (Nairobi –
Kenya) kwa msaada wao mkubwa wa kutafsiri kitabu hiki kutoka
kiingereza kwenda Kiswahili. Tunapenda kuwashukuru pia Dr T. M
Jafferji, Mkurugenzi Mtendaji, Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam, na
Mrs. Parul Chayya, Mtendaji Mkuu, TMJ Hospital, kwa kuunga mkono
kwa hali na mali na ushauri katika shughuli hii.
Natumaini wasomaji watakaopata kitabu hiki wataona umuhimu wake
na chenye kuelimisha. Mapendekezo yanakaribiswa ya kuboresha
kitabu hiki.
Tunawatakia wote afya njema.
Dr Gabriel L. Upunda
Dr Bashir Admani
Dr Sanjay Pandya
                         
                    
                       
                            
                            Kuhusu waandishi
    Dr Gabriel L. Upunda MD, M. Med; MPH
Dr G. L. Upunda alisomea Udaktari katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (1972), Alimaliza masomo ya uzamili katika Kutibu (Internal Medicine) mwaka 1978)  katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na mwaka 1993 alimaliza mafunzo ya uzamili (Masters in Pubic Health) huko Johns Hopkins School of Public Health, USA.
    Amekuwa Mganga wa Wilaya, Mganga wa Mkoa (mara mbili), na kwa zaidi ya miaka kumi na tano amekuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kama kiongozi wa Afya Ya Msingi, Mkurugenzi  wa Tiba na hatimae alikuwa Mganga Mkuu Wa Serikali kwa takriban miaka kumi. Dr G L Upunda amefanya kazi pia Shirika La Afya Ulimwenguni  (WHO - AFRO).
    Dr. Bashir Admani M.B.Ch.B, M. Med ((Paediatrics), C. Neph. (Paed)
 Dr Bashir Admani alimaliza mafunzo yake ya Udaktari (1998) na kufanya mafunzo ya uzamili katika fani ya watoto (2004) kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi, Kenya. Alipata mafunzo maalumu ya ubingwa wa juu katika magonjwa ya figo kwa watoto katika Red Cross Memorial Childrens’ ospital, Cape Town, Afrika ya Kusini. Sasa hivi anafanya kazi ya  Udaktari Bingwa wa  Figo kwa Watoto  katika Hospitali ya Chuo Kikuu Cha Aga Khan. Nairobi, Kenya. Yeye ni Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa  ya  Figo  kwa Watoto, Hospitali  ya Nairobi. Wakati tunapoandika  Dr Bashir Admani ni Katibu wa African Paediatric Nephrology Association (AFPNA).Aidha anatoa huduma zake pia kama Mweka Hazina wa Kenya Renal Association. 
                         
                    
                       
                            
                            Dr Sanjay Pandya
Dr Sanjay Panya ni Daktari Bingwa Mwandamizi wa Figo ambaye
anafanya kazi Rajkot ( Gujarat – India). “Kidney Education Foundation”
imeanzishwa naye ikiwa na kazi maalumu ya kusambaza ujumbe kwa
watu wengi ili kuzuia na kutibu magonjwa ya figo.Kitabu cha FIGO
kwa wagonjwa katika lugha za kiingereza, Hindi, Gujarat na Kutchi
kimeandikwa naye. Kwa kushirikiana na timu ya madaktari bingwa
kutoka sehemu mbalimbali duniani, vitabu vya kuelimisha wagonjwa
wa figo vimetayarishwa katika lugha zaidi ya 20.
Ili kuwasaidia watu na wagonjwa wa figo wengi zaidi sehemu mbalimbali
duniani,  Dr  Pandya  na  timu  yake  wameanzisha mtandao
www.KidneyEducation.com. Kupitia mtandao huu unaweza kuvipata
vitabu zaidi ya 230 katika zaidi ya lugha 20. Aidha katika miezi 60 watu
wameingia kwenye tuvuti hii  zaidi ya mara milioni 20.
Kwa hivi sasa kitabu hiki kwa wagonjwa  kinapatikana katika kiingereza,
kichina, kihispania, kijapani, kiitalia, kihindi, kiarabu, kireno, kibangla,
kiurdu na lugha nyingine kumi za kihindi.
                         
                    
                       
                            
                            
        Yaliyomo
        Sehemu 1:  Mambo ya misingi kuhusu figo
               
        
            | Sura ya 1 |  Utangulizi   | 1 | 
            | Sura ya 2 |  Figo na Kazi Yake   | 3 | 
            | Sura ya 3 |  Dalili za Magonjwa ya Figo   | 10 | 
            | Sura ya 4 |  Utambuzi wa Magonjwa ya Figo   | 13 | 
            | Sura ya 5 |  Magonjwa Makuu ya Figo   | 21 | 
            | Sura ya 6 |  Nadharia Potofu na Ukweli Juu ya Magonjwa ya Figo  | 27 | 
            | Sura ya 7 |  Kuzuia Magonjwa ya Figo  | 32 | 
        
        Sehemu 2: magonjwa makuu ya figo na matibabu
        figo Kushindwa
        
            | Sura ya 8  |  Kushindwa kwa Figo ni Nini?  | 39 | 
            | Sura ya 9  |  Kushindwa Ghafla kwa Figo  | 41 | 
            | Sura ya 10 |  Ugonjwa Sugu wa Figo: Chanzo  | 46 | 
            | Sura ya 11 |  Ugonjwa Sugu wa Figo: Dalili na Utambuzi | 48 | 
            | Sura ya 12 |  Ugonjwa Sugu wa Figo: Matibabu  | 55 | 
            | Sura ya 13 |  Dayalisisi  | 64 | 
            | Sura ya 14 |  Kubadilisha Figo | 86 | 
        
     
     
                         
                    
                       
                            
                            
    
        Magonjwa mengine makuu ya figo
        
            | Sura ya 15 |  Ugonjwa wa Kisukari wa Figo                   | 106 | 
            | Sura ya 16 |  Ugonjwa wa Figo wa Polisitiki(Polycystic)     | 115 | 
            | Sura ya 17 |  Kuishi na Figo Moja                           | 121 | 
            | Sura ya 18 |  Maambukizi ya Mfumo wa Mkojo                  | 124 | 
            | Sura ya 19 |  Ugonjwa wa Mawe Katika Figo                   | 131 | 
            | Sura ya 20 |  Uvimbe Usio wa Saratani kwenye Tezi Dume(BPH)   | 145 | 
            | Sura ya 21 |  Dawa ya Matatizo ya Figo                      | 157 | 
            | Sura ya 22 |  Nephrotic Syndrome                            | 162 | 
            | Sura ya 23 |  Maambukizi ya Mfumo wa Mkojo kwa Watoto       | 176 | 
            | Sura ya 24 |  Ugonjwa wa Kukojoa Kitandani                  | 188 | 
        
        Lishe   katika magonjwa ya figo
        
            | Sura ya 25 |  Lishe katika Ugonjwa Sugu wa Figo | 193 | 
             | Maelezo                                          |  210 | 
             | Vifupisho                                        |  218 | 
             | Vipimo vya Kawaida vya Damu Kwa Wagonjwa wa Figo |  220 | 
             | Ripoti                                           |  222 | 
        
 
                         
                    
                       
                            
                            Jinsi ya kutumia kitabu hiki
    Kitabu hiki kimo katika sehemu mbili
    Sehemu ya 1:
    
        Katika sehemu hii, ujumbe wa msingi juu ya figo na kujikinga na
        magonjwa ya figo yameelezwa. Kila mtu anashauriwa kusoma sehemu
        hii ya kitabu hiki..  Ujumbe uliotolewa waweza kukuletea mabadiliko
        kwa msomaji, kwa vile hunamuandaa msomaji wa kawaida kutambua
        na kujikinga na magonjwa ya figo.
    
    Sehemu ya 2:
    
        Msomaji anaweza kusoma sehemu hii kwa  kutaka tu kujua au ikiwa
        inabidi/ lazima.
    
    Katika sehemu hii
    
    - Ujumbe kuhusu magonjwa makuu ya figo, dalili, uchunguzi, kinga na matibabu yameshughulikiwa.
 
    - Magonjwa yanayoharibu figo kama kisukari, kupanda kwa damu / shinikizo la damu, polycystic kidney……nk) na tahadhari za kujikinga na ujumbe mwingi muhimu umeelezwa.
 
    - Maelezo ya ndani/maksusi kuhusu lishe bora kwa ugonjwa wa figo uliozidi.
 
    
    
        Ujumbe katika kitabu hiki sio matibabu Ya daktari;
        tiba bila ushauri wa Daktari huenda ikawa hatari.