Ugonjwa   wa  figo wa  uvimbe uliojaa maji (polycystic kidney disease - PKD).
Ugonjwa  huu  ndio ugonjwa  wa  figo  wa  kawaida  sana  ambao hurithiwa.Ni  ugonjwa wa figo kuvimba vibofu vingi vingi.Ndio  nambari ya  nne  kati ya vyanzo  vinavyosababisha ugonjwa sugu wa figo.Viungo vingine vya mwili vinavyoweza kupata vibofu hivi ni ini, ubongo, matumbo, kongosho, ovari  na wengu.
Matukio  ya vimbe za figo 
Ugonjwa wa vimbe za figo hupatikana kwa watu wa asili zote, wake kwa waume na humpata mtu mmoja kwa kila watu elfu duniani  kote.    karibu asilimia tano ya wagonjwa wote  wanaohitaji dayalisisi  au kupatiwa figo huwa na vimbe za figo.(PKD)
Figo  huathirika  vipi  na vimbe?(PKD) 
    - Figo  zote  mbili  huvimba  vibofu  vingi vingi  vilivyojaa  maji.
 
    - Vibofu hivi hutofautiana kwa ukubwa kuanzia vidogo kama sindano hadi vyenye upana wa hata sentimita kumi au zaidi.
 
    - Kadri muda  unavyo  endelea  vibofu huendelea kukua na polepole huendelea kufinya na kuharibu figo.
 
    - Uharibifu huu   husababisha   shinikizo la damu,  kuwepo  kwa protini kwenye mkojo na kazi za figo kudhoofika na mwishowe ugonjwa sugu wa figo hujitokeza.
 
    - Shida hii ikiendelea kwa muda mrefu figo huzidi  kudhoofika  (hadi ESKD) na huenda mgonjwa akahitaji  dayalisisi  au figo nyingine.
 
                         
                    
                       
                            
                            Dalili za ugonjwa wa figo kuvimba vibofu (PKD)
Watu wengi huishi miaka mingi bila dalili zozote.wengi huonyesha dalili baada ya umri wa miaka thelathini au arobaini. Dalili za kawaida ni:
    - Shinikizo la  damu.
 
    - Maumivu ya mgongo (upande mmoja au pande zote), mbavu , au tumbo    kuvimba.
 
    - Kuhisi uvimbe mkubwa tumboni.
 
    - Damu au protini kwenye mkojo.
 
    - Maambukizi  ya njia ya mkojo ya mara kwa mara na mawe ya figo.
 
    - Dalili za ugonjwa sugu wa figo jinsi figo zinavyoendelea kudhoofika.
 
    - Dalili zinazotokana na vimbe katika sehemu zingine za mwili kama ubongo, ini  au  kwenye matumbonk.
 
    - Matatizo ambayo mgonjwa anaweza kupata ni kama ubongo kuvimba (brain aneurysm), henia kwenye tumbo,ini  kupata maambukizi,  pochi sehemu ya mwisho ya utumbo (colon) na magonjwa ya moyo kwenye valve. Karibu asilimia kumi ya wagonjwa huvimba mishipa ya ubongo (aneurysm).Hali hii humfanya mtu aumwe na kichwa na kuwa katika hatari ya mshipa kupasuka na kusababisha kupooza na hata kifo.
 
Je,   ni  lazima  figo   zinazovimba vibofu zishindwe kufanya kazi? 
Hapana .Sio kila mgonjwa hupata ugonjwa wa kufeli kwa figo. Takriban asilimia hamsini hupata ugonjwa wa figo kufeli wakiwa na umri wa sitini,na kama asilimia sitini hupata wakiwa na miaka sabini.Wanaume sana sana ndio hufeli figo pia wanaopata vimbe hizi za figo wakiwa na  umri mdogo,walio na shinikizo la damu na protini au damu kwenye mkojo  pia huwa na figo kubwa.
PKD ni ugonjwa wa figo wa kurithi unaojulikana sana na ni wan ne kwa kuleta CKD.
                         
                    
                       
                            
                            Utambuzi wa vimbe za figo.(PKD)
Vipimo  vinavyotumika ni:
    - Ultrasound  ya  figo:  Kipimo  hiki  hutumika  sana  kwa  kuwa kinaaminika, rahisi, salama,hakina maumivu na kina gharama kidogo.
 
    - Picha za CT au MRI - Vipimo hivi huwa sahihi zaidi ingawaje ni ghali.Huweza kuonyesha vivimbe vidogovidogo kabisa ambavyo haviwezi kuonekana kwa picha ya ultrasound.
 
    - Familia kuchunguzwa; Vimbe za figo huwa ni ugonjwa unaorithiwa kwa wazazi na kila mtoto ana hatari ya kupata ugonjwa huu kwa kiasi cha 50:50.  Kwa hiyo, familia ya mgonjwa inafaa kupimwa mara moja.
 
    - Vipimo vya madhara ya vimbe kwenye figo:    Mkojo hupimwa ili kuchunguza uwepo wa damu au protini kwenye damu.  Kreatinini hupimwa ili kuchunguza na kufuatilia kazi ya figo.
 
    - Kutambuliwa  ugonjwa huu kwa bahati:  Vimbe za  figo zinaweza kuonekana kwa bahati mtu anapopimwa kawaida au anachunguzwa kwa picha za ultrasound kwa sababu nyingine.
 
    - Kuchunguza kuzingatia uhusiano wa kijeni au kidamu (gene tests). kipimo hiki hutumiwa kuchunguza ni nani kwenye familia ana jeni za ugonjwa huu.kipimo hiki kinafaa kutumiwa iwapo vipimo vya picha havionyeshi chochote.Kipimo  huwa kinapatikana  katika vituo vichache na ni ghali sana.
 
Kwa    familia ni nani   afaa kupimwa kuchunguza vimbe za figo? 
Ndugu na watoto wa mgonjwa wanafaa kupimwa. Pia ndugu wa wazazi wa mgonjwa.
Je, ni watoto  wote wa mgonjwa wako katika hatari ya kupata vimbe za  figo? 
La,vimbe za  figo ni ugonjwa unaorithiwa  iwapo baba au mama anao,watoto wana uwezekano wa asilimia hamsini ya kuupata pia.
Maumivu ya mbavu na mgongo au damu kwenye mkojo katika umri wa arobaini huwa dalili ya vimbe kwenye figo.
                         
                    
                       
                            
                            Kuzuia vimbe za figo
Kupunguza vimbe za figo:
Familia yote kupimwa mapema kabla ya ugonjwa  kuanza  kuna faida nyingi.  Ugonjwa unapojulikana mapema, huweza kutibiwa vyema zaidi. Kutambua na kutibu  shinikizo la damu huzuia kuendelea au kuzidi kwa figo kudhoofika.Kubadili mienendo na vyakula kwa wagonjwa wa vimbe za figo hukinga figo zao na pia moyo.Ubaya wa kupimwa ni kwamba mtu anaweza kushikwa na wasiwasi ilhali hana dalili zozote na hata hahitaji matibabu yoyote.
Kwa nini ni vigumu kupunguza matukio ya  vimbe za figo? 
Ugonjwa  huu kwa kawaida hutambuliwa katika umri wa miaka arobaini au zaidi.Wengi huwa na watoto kabla ya umri huu na  hivyo vigumu kuzuia kupitia kwa vizazi.
PKD ni ugonjwa wa figo wa kurithi, kwa hiyo ni vyema kuwapima watu wazima wote wa familia hiyo ili kuona kama yeyote ana PKD.
                         
                    
                       
                            
                            Matibabu  ya  vimbe   za  figo
- Vimbe  za  figo  hauna  tiba ya kuponesha lakini huhitaji matibabu ili
kulinda figo  na kuzuia kukua kwa ugonjwa sugu wa figo hadi kufikia
kipindi chake cha mwisho (ESKD)hivyo nia iwe kuendeleza uhai.
 - Kuzuia dalili na matatizo yanayoweza kuambatana na hali hii
(complications).
 
Mambo muhimu katika matibabu ya vimbe za figo:
- Mgonjwa huwa hana dalili zozote kwa  miaka mingi baada ya
ugonjwa kutambulika,na hivyo hahitaji matibabu yoyote. Wagonjwa
kama hawa huhitaji kuangaliwa na daktari mara kwa mara.
 - Kuhakikisha kuwa shinikizo la damu limezuiliwa  na hivyo  kupunguza
kasi ya ugonjwa sugu wa figo.
 - Kuzuia maumivu kwa dawa ambazo hazidhuru figo kama vile aspirin
au acetaminophen . Inawezekana  kukawa na maumivu ya mara
kwa mara au hata wakati wote. Hii ni kwa sababu vimbe zinakua.
 - Kutibu mara moja maambukizi ya njia ya mkojo kwa kutumia dawa
za antibayotiki zinazofaa.
 - Kutibu mawe ya figo mapema.
 - Kunywa vinywaji kwa wingi  kama mgonjwa hajavimba.Hii huzuia
maambukizi  ya njia ya mkojo na mawe ya figo.
 - Matibabu bora ya ugonjwa sugu wa figo kama ulivyoelezwa  katika
sura ya 10-14.
 - Kwa wagonjwa wachache vibofu  hupasuliwa ili kuvitoa maji kwa
sababu ya maumivu, kutokwa na damu,maambukizi au njia ya mkojo
kufunga.
 
Matibabu hulenga kupunguza kuendelea kwa ugonjwa sugu wa figo,
kutibu maambukizi ya figo, mawe ya figo na maumivu tumboni.
                         
                    
                       
                            
                            Je, mgonjwa wa vimbe za figo anafaa kumwona daktari lini?
Mgonjwa anafaa kumwona daktari mara moja iwapo:
- Ana  homa,maumivu ya tumboni ya ghafla au mkojo mwekundu.
 - Maumivu makali  au yanayo jirudia rudia ya kichwa.
 - Kujeruhiwa figo au figo kuongezeka ukubwa.
 - Maumivu ya kifua, kukosa hamu ya chakula, kutapika sana, misuli
kukosa nguvu,kuchanganyikiwa , kusinzia au kuzimia.
 
Mgonjwa ambaye hana dalili anaweza kukaa kwa miaka
mingi bila ya kuhitaji matibabu.